• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 12:38 PM
United Bank for Africa yafanya usafi jijini Nairobi

United Bank for Africa yafanya usafi jijini Nairobi

Na GEOFFREY ANENE

HUKU jiji la Nairobi likikabiliwa na changamoto jinsi ya kukabiliana na utupaji wa taka, benki ya United Bank for Africa (UBA) iliamua kufanya usafi kwenye barabara ya Moi Avenue, Jumamosi.

Ikiongozwa na Afisa Mkuu Mtendaji wa Benki hiyo wa eneo la Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika, Emeke Iweriebor, wafanyakazi wa benki hiyo kutoka matawi yote nchini, wamesafisha eneo kati ya bustani ya Jeevanjee na jengo la Union Towers katikati mwa jiji.

Wafanyakazi wa United Bank for Africa (UBA) wafanya usafi jijini Nairobi, Jumamosi, Septemba 14, 2019. Picha/ Geoffrey Anene

“Hii ni sehemu ya mradi wetu wa kusafisha jiji. Tunashirikiana na serikali ya kaunti ya Nairobi kurembesha jiji na kuhamasisha wakazi kuhusu umuhimu wa usafi na njia salama za kulinda mazingira,” amesema Iweriebor.

Raia huyo wa Nigeria aliongeza kuwa benki hiyo itaendelea kusaidia miradi ambayo jamii imeweka ya kukabiliana na utupaji wa takataka.

Kuifanya shughuli kuwa mazoea

Ikiwa ni mara ya kwanza ya benki hiyo kujihusisha na usafishaji wa jiji, Iweriebor amehakikishia wakazi wa Nairobi kuwa wataendeleza shughuli hiyo mara kwa mara sio katkati mwa jiji tu, bali pia katika maeneo tofauti jijini.

“Mbali na lengo letu la kutoa huduma za benki, tunataka kujihusisha katika ufanisi wa jamii tunazojihudumia kwa njia tofauti ikiwa ni pamoja na kuchangia katika kuimarisha mazingira, michezo na kadhalika,” amesema afisa huyo baada ya kusafisha sehemu hiyo ya barabara hiyo yenye umbali wa kilomita moja.

Utupaji wa taka chini ya daraja Korogocho jijini Nairobi. Benki ya United Bank for Africa ilifanya usafi kwenye barabara ya Moi Avenue mnamo Septemba 14, 2019. Picha/ Geoffrey Anene

You can share this post!

SHANGAZI AKUJIBU: Kipusa anayetosha mboga haamini...

DAU LA MAISHA: Usimuone mdogo wa mwili ukamdharau…

adminleo