• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 8:55 PM
Wanahabari 3 wa NMG watambuliwa na Rais

Wanahabari 3 wa NMG watambuliwa na Rais

Na LUCY KILALO

WANAHABARI watatu wa shirika la Nation Media Group, Nasibo Kabale, Vera Okeyo na Angela Oketch ni miongoni mwa watu waliotambuliwa na Rais Uhuru Kenyatta kwa uzalendo wao.

Waandishi hao wa masuala ya afya, wamekuwa katika mstari wa mbele katika uandishi wa taarifa kuhusiana na maambukizi ya virusi vya corona miongoni mwa masuala mengine ya kiafya.

Wanahabari wengine kadhaa kutoka kwa mashirika mbalimbali ya habari pia walitambuliwa kupitia kwa tuzo hiyo.

“Kwa kufanya zaidi ya wajibu wao wa kujuza, kuelimisha na kuhamasisha Wakenya kuhusu ugonjwa wa Covid 19, mara nyingi wakiwa wanahatarisha afya yao wenyewe, wanahabari hawa wameonyesha uzalendo wa kweli na kujipatia tuzo kuu la kitaifa,” taarifa hiyo ilieleza.

Mkurugenzi Mkuu wa Afya, Dkt Patrick Amoth aliyekuwa pia kati ya maafisa wa afya ambao wanaongoza katika kushughulikia janga la corona nchini, pia alituzwa. Madaktari wengine kadha pia walitambuliwa kwa juhudi zao katika kukabiliana na maambukizi ya maradhi yanayotokana na virusi hivyo.

 

You can share this post!

Refarenda yaja

Rais adokeza kuhusu shule na makanisa kufunguliwa

adminleo