• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 6:47 PM
Washukiwa wa ukahaba jijini walala fofofo kortini

Washukiwa wa ukahaba jijini walala fofofo kortini

Na RICHARD MUNGUTI

MWANAMKE (pichani) aliyekuwa miongoni mwa wachuuzi zaidi ya 200 waliokamatwa wakikaidi sheria za kaunti ya Nairobi alilala fofofo kortini akisubiri kesi inayombakili itajwe.

Sio mwanamke huyu aliyelala kortini peke yake bali ni wengi.

Washtakiwa walikoroma kwa kuzidiwa ni usingizi  hakimu alipochelewa kufika kuendelea na kesi zilizowakabili.

Hakimu alipoingia mahakamani, meza iligongwa kisha washukiwa wote wakasimama huku waliokuwa wamezama katika lindi la usingzi wakifuta matongo machoni.

Walitozwa faini ya kati ya Sh500 hadi Sh3000 kwa makosa ya kuendeleza ukahaba, kutupa chafu kwenye barabara na pia kuuza bidhaa mahala wasiporuhusiwa.

You can share this post!

Wazir kujua hatima yake Alhamisi

‘Wazir kipenzi cha wabunge wanawake si...

adminleo