• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 2:53 PM
Alilamba vya pembeni, sasa hana ‘transfoma’ baada ya mke kuikata kwa makasi

Alilamba vya pembeni, sasa hana ‘transfoma’ baada ya mke kuikata kwa makasi

Na MASHIRIKA

FENGCHENG, UCHINA

MWANAMUME anauguza majeraha mabaya baada ya mke wake kumkata uume wake.

Inasemekana mwanamke huyo alishuku mume wake ana mpenzi wa kando ndiposa akachukua makasi na kumkata uume.

Kulingana na mashirika ya habari Uchina, mwanamume huyo alikuwa akipiga mswaki wakati mke wake alipomshambulia ghafla. Walikuwa wamebishana awali lakini hakujua mke wake alikuwa bado ana hasira.

Duru katika hospitali ambako mwanamume huyo aliyetambuliwa kama Li alillazwa zilisema alifikishwa huko akivuja damu jingi.

Mashirika ya habari yalimnukuu akisema kuwa mke wake alikuwa akimshuku sana.

Ilidaiwa alisema mke wake alimpiga marufuku kuzungumza na rafiki yeyote wa kike wala hata kutabasamu na mwanamke kwa mbali.

Ingawa wamekuwa wakibishana mara kwa mara, hakutarajia kuna siku ingefika ambapo mke wake angemkata uume wake.

Madaktari walinukuliwa kusema alifanyiwa upasuaji wa dharura kuokoa maisha yake lakini hawezi kuhakikishiwa atarejelea hali yake ya kawaida ya udume atakapopata nafuu.

-Imekusanywa na Valentine Obara

You can share this post!

Wanandoa wanyweshwa mkojo kwa kuoana kisiri

Wachumba wamwagiwa kinyesi kwa kula uroda nje ya ndoa

adminleo