• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:55 AM
Kioja cha mwaka kichwa cha mume kukwama ndani ya uke wa mkewe

Kioja cha mwaka kichwa cha mume kukwama ndani ya uke wa mkewe

MASHIRIKA Na PETER MBURU

KILIKUWA kioja cha mwaka pale wanandoa nchini Amerika walipelekwa hospitalini katika hali mbaya, baada ya kichwa cha mume kukwama katika uke wa mkewe, katika hali isiyoeleweka.

Wanandoa hao wanasemekana kuwa walikuwa wakishiriki ngono, japo bado haijafamika ni ngono ya aina gani.

Tom na mkewe Janis Morrison, wanandoa kutoka mji wa Greensboro, Alabama wanaripotiwa kupigia simu namba ya dharura 911 saa nne usiku, wakiomba msaada wa ambulensi ya kuwapeleka hospitalini.

Samantha Irving ambaye alipokea simu hiyo, hata hivyo, alisema aliona kama ulikuwa mzaha alipoambiwa tatizo.

“Mwanamke huyo aliniambia kuwa mumewe alikuwa ameanguka na kuwa kichwa chake kilikuwa kimekwama katika uke wake. Nilidhani ni matineja ambao walikuwa wakisumbua,” akasema Irving.

Lakini licha ya shauku yake, Irving alituma ambulensi nyumbani kwa wanandoa hao, ambapo madaktari walibaini kuwa ilikuwa ukweli.

Madaktari hao walisema kuwa waliwapata wawili hao wakiwa uchi kitandani, huku damu ikiwa imetapakaa.

“Mwanamke alikuwa akipiga nduru sana kila mwanamume aliposonga, lakini nusu ya uso wake ulikuwa umekwama ndani na alionekana kuwa anayeumia,” akasema mmoja wa madaktari.

Walikimbizwa katika hospitali ya karibu, ambapo walihudumiwa na kutenganishwa.

Morrison aliathirika kwa kuvuja damu ndani ya mwili, naye mumewe akapata majeraha machache usoni.

Visa vya aina hiyo havijakuwa vikishuhudiwa mara nyingi US, ila tu vile vya wanawake na wanaume kukwamiana wanapofanya ngono ya kawaida.

You can share this post!

Siasa hizi zitawaponza, Sudi awaambia Matiang’i na...

AKILIMALI: Wafugaji waungana kuanzisha kiwanda chao cha...

adminleo