Habari

Kindiki ataka Sh450m zaidi za helikopta na chakula afisini mwake

Na DAVID MWERE March 24th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

AFISI ya Naibu Rais Profesa Kithure Kindiki inataka Sh450 milioni kulipia shughuli za kila siku za afisi yake pamoja na kukodisha helikopta kulingana na stakabadhi kabla ya Bunge la Kitaifa.

Afisi ya Profesa Kindiki awali ilikuwa imetengewa Sh523 milioni kugharimia shughuli hizo.

Anataka Sh350 milioni zaidi ambayo itafikisha bajeti zima ya afisi yake mwaka huu hadi Sh873 milioni kabla ya kukamilika kwa mwaka wa kifedha unaokamilika Juni.

Gharama ya afisi yake ni chakula pamoja na burudani.

Mbunge wa Kisumu Magharibi Rosa Buyu alishutumu mgao mkubwa kwa afisi ya naibu rais akisema unaenda kinyume na wito wa Rais William Ruto wa kubana matumizi ya serikali.