Gavana wa Kisii, Simba Arati alipowasili Kenyenya, Bomachoge kuongoza wananchi kuadhimisha Madaraka Dei 2026 mnamo Juni 1. Picha|Wycliffe Nyaberi
KIHISTORIA, kando na maadhimisho ya Madaraka Dei kila mwaka kuongozwa na Rais wa nchi, sherehe hiyo pia hufanyika kwenye kaunti aidha chini ya Gavana au Kamishna wa Kaunti.
Gavana akiwakilisha serikali ya kaunti na kuhutubia umma, Kamishna wa Kaunti anawakilisha serikali ya kitaifa na husoma hotuba ya kitaifa ya Rais. Kwenye maadhimisho ya mwaka 2026 ya Madaraka Dei, baadhi ya kaunti zilisherehekea sikukuu ya Kenya kupata utawala wa ndani kwa ndani.
Zifuatazo ni picha kutoka Kaunti ya Homa Bay na Kisii;
Gavana wa Kisii, Simba Arati alipowasili Kenyenya, Bomachoge kuongoza wananchi kuadhimisha Madaraka Dei 2026 mnamo Juni 1. Picha|Wycliffe NyaberiGwaride na maafisa wa polisi Kisii. Picha|Wycliffe NyaberiKamishna wa Kaunti Homa Bay akipiga saluti wakati wa maadhimisho ya Madaraka Dei, Juni 1, 2026. Picha|George OdiwuorWanafunzi kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Bongu wakicheza densi ya Kihindi wakati wa maadhimisho ya siku ya Madaraka 2026, Juni 1, katika uwanja wa Rapedhi, Ndhiwa, Kaunti ya Homa Bay. Picha|George Odiwuor