Serikali yapunguza viwango vya ubora wa mafuta ‘kuzuia uhaba’
SERIKALI imetangaza kupunguza viwango vya ubora wa mafuta yanayouzwa nchini, kwa kuruhusu madini hatari ya Sulphur kuongezwa kwa kipindi cha miezi sita.
Katika taarifa iliyotolewa na Waziri wa Biashara na Uwekezaji Lee Kinyanjui, serikali inasema wameafikia kuongeza viwango vya Sulphur hadi miligramu 50 kwa kilo katika dizeli na petrol baada ya mashauriano na vitengo mbali mbali vya kiufundi.
Waziri Kinyanjui anasema hatua hiyo inatokana na vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati na haswa mzozo wa kufungwa kwa Mkondo wa Hormuz ambao umeathiri usambazaji wa mafuta kutoka nchi za ghuba.
“Hatua inanuiwa kuhakikisha kwamba taifa litaendelea kuwa na mafuta ili kuleta uthabiti wa kiuchumi wakati huu ambapo kuna mgogoro kuhusu upatikanaji wa bidhaa hii,” ikasema taarifa ya Waziri Kinyanjui aliyotundika katika safu yake hapa.