Dimba

Kisura Brooke atishia kuvunjia De Bruyne ndoa

Na CHRIS ADUNGO July 20th, 2024 2 min read

MICHELE Lacroix ambaye ni mke wa Kevin de Bruyne ametishia kuvua pete yake ya ndoa iwapo kiungo huyo matata wa Manchester City, Kevin de Bruyne, hatamzuia kahaba Elle Brooke kumfikia mitandaoni.

Elle, ambaye ni shabiki sugu wa Man-City, alitoa ahadi ya kumfungulia De Bruyne mzinga wake wa asali mwezi huu iwapo sogora huyo mzoefu angechochea timu ya taifa ya Ubelgiji kunyanyua taji la Euro 2024 nchini Ujerumani. Hata hivyo, Ubelgiji walidenguliwa mapema na Ufaransa kwa 1-0 katika hatua ya 16-bora.

Demu huyo, ambaye pia ni bondia na mwamamitindo, aliwahi pia kufichua mapenzi yake kwa De Bruyne msimu jana baada ya jaribio lake la kumtia Erling Haaland kishawishini kugonga mwamba.

“Itakuwa burudani chumbani kwa KDB iwapo atafaulu kutuongoza kushinda EPL, FA na UEFA,” akaandika mrembo huyo kwenye Instagram akiwa amevalia jezi ya Man-City waliokosa kutia kibindoni ufalme wa UEFA.

Elle pia aliapa kuvua nguo na kusalia uchi wa mnyama iwapo De Bruyne angetawazwa Kiungo Bora, Mfungaji Bora au Mchezaji Bora wa EPL mwishoni mwa muhula wa 2023-24.

“Lazima nimuonyeshe anachokikosa kwa mkewe kabla ya kumpa kabisa ufunguo wa mzinga huu wa asali,” akaandika kwenye Instagram.

Kilichomkoroga nyongo zaidi Michele majuzi ni video fupi iliyopakiwa na Elle mitandaoni akitamtaka De Bruyne afanye hima na kuenda kutikisa maziwa na makalio yake. Video hiyo ilitazamwa na mashabiki 63,000 wa mrembo huyo kwenye Instagram chini ya saa moja.

Michele alianza kutoka kimapenzi na De Bruyne mnamo 2014, miezi michache baada ya kiungo huyo kurushiana makonde na mchezaji mwenzake kambini mwa Ubelgiji, kipa Thibaut Courtois.

Wakati huo, aliyekuwa demu wa De Bruyne, Caroline Linjen, alikuwa ameanza kumwonjesha tunda Courtois ambaye kwa sasa anadakia Real Madrid ya Uhispania.

De Bruyne alimvisha Michele pete ya uchumba Desemba 2016 na wakafunga pingu za maisha Juni 2017. Ndoa yao imejaliwa watoto watatu – Mason, Surri na Rome.

Mwanzoni mwa mwaka huu, mwanamitindo maarufu mzawa wa Uingereza, Joanne Parker ambaye ni mama wa watoto wawili, mwandishi na mfanyabiashara maarufu jijini London, naye alipasua mbarika na kufichua alivyomburudisha De Bruyne kimapenzi mnamo 2018.