• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 5:45 AM
Lazima tuzime mashambulizi ya Liverpool, asema Guardiola

Lazima tuzime mashambulizi ya Liverpool, asema Guardiola

Na CHRIS ADUNGO

MAN City wanaikaribisha Liverpool uwanjani Etihad kujaribu kubadilisha kibao cha ushindi wa 3-0 wa vijana wa Jurgen Klopp ugani Anfield.

Lakini ikiwa wenyeji hao watapigwa bao moja tu na Liverpool, watajua itawabidi wafunge mabao matano ili kufuzu kwa nusu fainali.

Na kocha wao Pep Guardiola anajua uzito wa kazi iliyopo Jumanne usiku akiwa mzoefu wa michezo ya Klabu Bingwa Ulaya.

“Ili kufuzu, unafaa kucheza soka safi bila makosa” akasema kocha huyo katika kikao na wanahabari Jumatatu.

“Tunahitaji kuunda nafasi za kufunga na kuhakikisha tumezima nafasi ya kufungwa. Mashambulizi ya Liverpool lazima tuyakabili kikweli.

“Tuna dakika 90 pekee na chochote cheza kutokea. Tunakachofanya ni kujaribu kushinnda.

 

“Tutafikiria kuhusu idadi ya mabao tutakayofunga baada ya kupata bao la kwanza.”

Naye kiungo mkabaji wa timu hiyo Fernandinho amesema ni jukumu lake pamoja na wachezaji wazoefu kuiinua Man City ambayo imepokea vichapo viwili ndani ya siku nne kwa mara ya kwanza msimu huu.

“Imekuwa wiki ngumu kwetu, vichapo viwili, lakini haya kwa sasa ni ya kale,” akasema Mbrazili huyo na kuongeza kuwa ili washinde, lazima wawe na matumaini.

You can share this post!

Msiidhalilishe Man City, Klopp aonya

John Baraza sasa kuwaongoza ‘Batoto Ba Mungu’

adminleo