Mbio za The Great Murang’a Community Run kufanyika kwa mara ya kwanza mwezi huu
KAUNTI ya Murang’a itakuwa mwenyeji wa mashindano ya kwanza ya riadha ya The Great Murang’a Community Run, tarehe 31 mwezi huu.
Hili ni shindano la kwanza la aina yake katika kaunti hiyo, likilenga kukuza vipaji na kuhamasisha jamii kuwa na afya bora.
Uzinduzi rasmi wa tukio hili kwa vyombo vya habari, ulifanyika Alhamisi katika kaunti hiyo na ulifanywa rasmi na Katibu wa Michezo, Elijah Mwangi na viongozi mbalimbali kutoka shirikisho la Riadha Kenya (AK), wanariadha mashuhuri kutoka Murang’a, pamoja na wawakilishi wa sekta binafsi na taasisi za kifedha, ikiwemo NACADA.
Lengo kuu la mbio hizi ni kupambana na matumizi ya dawa za kulevya miongoni mwa vijana, huku pia zikitumika kama jukwaa la kutambua na kukuza vipaji vya riadha.
Mbio hizi zitakuwa za aina mbalimbali kama; kilomita 10 (wanawawake na wanaume), kilomita 8 (wanaume wasiozidi miaka 20), kilomita 6 (wanawake wasiozidi miaka 20), kilomita 2 (miaka kati ya 13-15 na 50-60), kilomita 1 (watoto kati ya miaka 9-12) na mita 500 watu wenye umri ziadi ya 61 bila malipo.
Kila mmoja ambaye atashiriki mbio za kilomita 5 kwa taasisi za kifedha na mbio za kilimita 2 kwa familia, watalipa Sh 1,000.
Kupitia ushirikiano wa wadau mbalimbali, Great Murang’a Community Run inatarajiwa kukuza uchumi.
Zaidi ya kuwa sherehe ya riadha, tukio hili pia litatoa fursa ya kuuza Murang’a kama kitovu cha michezo na kivutio cha utalii, sawa na utajiri wake wa kilimo.