Habari Mseto

Polisi wawakamata wawili na gunia 10 ya bangi Diani

Na JURGEN NAMBEKA September 21st, 2024 1 min read

POLISI kutoka Kaunti ya Kwale wanawazuilia watu wawili waliokamatwa mjini Diani wakiwa na magunia 10 ya misokoto ya bangi.

Kwa mujibu wa ripoti ya polisi, oparesheni hiyo iliyofanyika Septemba 20 na kikosi cha kukabiliana na ulanguzi kilichoongozwa na Naibu Kamishna wa kauntyi Bw Josphat Mutisya, polisi walipata habari kuhusu nyumba moja katika eneo la kibiashara la Kona Musa.

Bw Hamisi Omari aliyekuwa akiishi kwenye nyumba hiyo, alikamatwa katika eneo la tukio na akawaelekeza polisi kwa nyumba nyingine ambako Mwanamke kwa jina Bi Ikoye Auma alikamatwa.

Alikuwa akishukiwa kuhusika katika kusafirisha dawa za kulevya kutoka Mombasa hadi Diani.

“Washukiwa wamefikishwa katika kituo cha Polisi cha Diani na kuwasilishwa kwa maafisa wa uchunguzi wa makosa ya jinai (DCI) Mombasa kwa uchunguzi zaidi,” ikasema ripoti hiyo.