Dondoo

Polo akosa kuoga siku tatu kuadhibu mkewe


NAKURU MJINI

JAMAA wa hapa aliwavunja wenzake mbavu kwa kicheko alipokiri kuwa, alikosa kuoga kwa siku tatu mkewe alipodinda kumbebea maji kwenye bafu.

Duru zinasema jamaa alikosana na mkewe alipodinda kumpa hela za saluni.

Inasemekana kalameni alimpa kidosho pesa za matumizi lakini akataka zaidi akilia alifanya bajeti na kugundua hana ya saluni.

“Jamaa hakumsikiliza naye mrembo akadinda kumpa huduma kadhaa,” mdokezi wetu alifichua.

 

Jamaa asalia uchi wa mnyama baada ya kufyonzwa na makuro danguroni

BOMET MJINI

MWANAUME mmoja alizua sokomoko katika eneo hili alipovua nguo zake zote na kusalia uchi wa mnyama.

Hii ni baada ya kuibiwa hela zote alizokuwa amelipwa na kiwanda cha sukari ambapo anapeleka na kuuza miwa yake.

Inasemekana mzee huyo alikuwa amelipwa Sh500,000 baada ya kuwasilisha miwa kwa muda.

Kulingana na mdokezi, jamaa wa watu aliamua kuingia nyumbani kwa mama pima akiwa na Sh490,000 kabla yake kudai vijana aliokuwa amewanunulia pombe walikuwa wamemwibia hela zote.

Waliofika kujua kilichotokea walishangaa ni kwa nini alikuwa ameenda kulewa akiwa na hela hizo nyingi hivyo.

“Mama mmoja aliamua kumpa Mzee huyo ushauri ila akadinda kwenda nyumbani akidai huenda mkewe hangeamini amrporwa mapato yake yote ya mwaka mzima,”alisema mdokezi.