Mkasa wa moto: Methu afoka, ataka Ogamba na Murkomen wajiuzulu
SENETA wa Nyandarua, John Methu alimchemkia Waziri wa Elimu Julius Ogamba na Waziri wa Usalama wa Ndani Kipchumba Murkomen akitaka wajiuzulu kufuatia mkasa wa moto katika Shule ya Wasichana ya Utumishi Academy uliosababisha vifo vya wanafunzi 16.
Akizungumza kwa mara ya kwanza kama Kaimu Katibu Mkuu wa DCP, Bw Methu alishutumu serikali kwa uzembe, ukosefu wa uwezo na kushindwa kujiandaa kukabiliana na majanga.
Methu alisema taifa limeendelea kushuhudia majanga shuleni kwa miaka mingi bila mageuzi ya maana kufanywa kuwalinda wanafunzi wa shule za bweni.
Seneta huyo alikosoa serikali kwa jinsi ilivyoshughulikia mkasa wa moto katika Shule ya Utumishi Academy akidai maafisa wakuu walichelewa kuchukua hatua licha ya kupokea taarifa mapema kuhusu janga hilo.
“Tunafahamu wazi kuwa Waziri wa Usalama wa Ndani Kipchumba Murkomen aliarifiwa kuhusu mkasa huo saa nane usiku lakini hakuweza kuelekeza vyombo vya serikali na kusafiri umbali wa saa moja na nusu,” alisema Methu.
Kwa mujibu wa Methu, Murkomen anapaswa kuwajibika binafsi kwa vifo vya wanafunzi hao.
Chama hicho cha upinzani pia kilishutumu serikali ya Kenya Kwanza kwa kudhoofisha mifumo ya kitaifa ya kukabiliana na majanga kwa kuhamisha majukumu muhimu kutoka taasisi rasmi hadi kwa watu binafsi.
Aidha, chama hicho kilimlaumu Waziri wa Elimu Julius Ogamba kwa kutofika mara moja eneo la tukio baada ya mkasa huo.
DCP ilidai kuwa kama serikali ingetumia nguvu sawa katika usimamizi.