Kimataifa

China kutuma kundi la wataalamu DRC kusaidia kudhibiti Ebola

Na REUTERS June 1st, 2026 Kusoma ni dakika: 1

BEIJING, China

CHINA itatuma kundi la wataalamu wa kimatibabu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kupiga jeki juhudi za kudhibiti mlipuko wa Ebola, msemaji wa Wizara ya Masuala ya Kigeni Lin Jian alisema jana.

“Serikali ya China imeamua kutoa usaidizi wa kibinadamu kwa taifa la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na itaendelea kufanya hivyo kwa njia bora inavyoweza,” Lin akaongeza.

Wakati huo huo, wauguzi wanne ambao walikuwa wakitibiwa Ebola inayosababishwa na aina ya virusi kwa jina ‘Bundibugyo’ wameruhusiwa kuondoka katika hospitali moja mjini Bunia baada ya kupata afueni, kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO).

Wengi wanatarajiwa kupona haswa watu wanapofanyiwa ukaguzi wa kiafya mapema na wapate huduma za matibabu, huku juhudi za kudhibiti msambao wa ugonjwa huo zikiendelea kushika kasi.