Mudavadi: Ruto atashinda kwa kura asilimia 70 mpaka iwe vigumu kupeleka kesi kortini
KINARA wa Mawaziri Musalia Mudavadi ameonyesha imani yake kuwa Rais William Ruto atashinda 2027 kwa zaidi ya asilimia 70.
Akiongea kwenye mahojiano na kituo kimoja nchini Jumatatu, Mei 11, 2026, Mudavadi alisema wataendesha kampeni kali ambayo itahakikisha rais anashinda kwa kura nyingi kiasi kuwa upinzani hata utaaibika kuelekea kortini.
Alisema pengo kubwa la ushindi litaonyesha kuwa umma una imani na utendakazi wa serikali ya Kenya Kwanza.
Bw Mudavadi alisema kuwa kumekuwa na kesi za kupinga matokeo ya urais kwa sababu ya mwanya mdogo wa ushindi kati ya wawaniaji wakuu wa urais.