• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
Kalameni aangushia mama yake mijeledi akidai anamchafulia mkewe sifa

Kalameni aangushia mama yake mijeledi akidai anamchafulia mkewe sifa

Na JOHN MUSYOKI

Jamaa mmoja mjini hapa alishangaza watu kwa kutoogopa laana na kumwangushia mamake viboko. Hii ni baada ya kushutumu kwa kumchafulia sifa mkewe akidai ni mshirikina.

Inasemekana jamaa alipandwa na mori na kumtandika mamake bila huruma hatua ambayo iliwakera watu.

“Hata kama wewe ni mamamgu sitakubali uharibie mke wangu jina kwa kusema yeye ni mshirikina,” jamaa alisema huku akimtandika mamake.

Inasemekana jamaa alizidi kumwangushia kichapo licha ya mamake kulia amhurumie

Nusura umati umchukulie jamaa hatua kwa kushambulia mamake lakini jombi alikamatwa na kushtakiwa kwa kumtishia mamake maisha kando na kumjeruhi.

Jamaa alipokamatwa alijutia hasira zake zilizopelekea kumtandika mamake kwa kudai mkewe alikuwa anashiriki vitendo vya ushirikina bila kuthibitisha iwapo madai hayo yalikuwa ya kweli.

***

Ajuza ashangaza kudai hajawahi kulamba asali

PERTH, AUSTRALIA

Na DAILY MAIL

Bikizee mmoja mjini hapa mwenye umri wa miaka 68, aliacha waumini wa kanisa moja katika hali ya mshangao mkubwa kwa kufichua kwamba, hajawahi kufanya mapenzi na mwanamume katika maisha yake.

Katika ushuhuda ambao baadhi ya watu waliokuwepo walitilia shaka, mama huyo ambaye hana watoto na ni mtaalamu wa masuala ya ukarimu alisema katika umri wake angali bikira.

“Inawezekana kudhibiti hisia zako. Mimi nimekuwa bikira hadi sasa na sio eti ni kwa sababu niko na kasoro ya kimwili.
Ni kujichunga kwa sababu wanaume wanapenda kutumia wanawake vibaya,” alisema na kutaka wanaotilia shaka waandamane naye kwa wataalamu wakathibitishe hilo.

Tukio hilo lilizua gumzo kubwa mtaani wengi wakishangaa alivyoweza kudhibiti hisia zake kwa muda huo wote.

***

Arobaini za pasta fisi zagonga aliponaswa akimezea ‘mali’ ya mtu

RABAI, KILIFI

Na JANET KAVUNGA

Tabia ya ufisi ya mhubiri wa hapa ilimfanya ajute majirani wa mke wa mtu aliyenyemelea walipoanika vitendo vyake. Pasta huyo alikuwa akitembelea wanawake akidai alitaka kuwaombea.

Juzi alifika kwa mwanamke ambaye mumewe alikuwa amesafiri nje ya nchi na akaandaliwa mlo kabla ya kumpapasa bila kujua majirani walikuwa wamemwekea mtego.

“Bakini hivyo hivyo msiogope. Kanisa lote litajua yale unayofanya na wake za watu,” mzee mmoja aliyekuwa akichungulia kwenye dirisha alinguruma kabla ya majirani wengine kufika na kumuaibisba pasta kwa kuwaita wazee wa kanisa lake kushuhudia.

  • Tags

You can share this post!

KNEC yakiri kulikuwa na dosari katika matokeo ya KCPE

Miili ya vibarua watatu waliozama majini wakizibua mtaro...

T L