• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Nakumatt yamumunywa kama pipi na Nkana ya Zambia

Nakumatt yamumunywa kama pipi na Nkana ya Zambia

Na GEOFFREY ANENE

NAKUMATT FC imelimwa 4-0 na miamba wa Zambia, Nkana, katika mechi ya kirafiki uwanjani Camp Toyoyo, Nairobi, Jumatatu.

Klabu hii inayoshikilia nafasi ya tisa kwenye Ligi Kuu ya Kenya, ilifungwa mabao mawili katika kila kipindi.

Walter Bwalya aliweka Nkana bao 1-0 juu dakika ya 37 kabla ya mabingwa mara 12 wa Zambia kuenda mapumzikoni 2-0 mbele Idris Mbombo alipoongeza bao la pili dakika ya 42. Jacob Ngulube alimega pasi zilizofungwa na Bwalya na Mbombo.

Festus Mbewe aliimarisha uongozi hadi 3-0 dakika ya 61 baada ya kupokea pasi nzuri kutoka kwa Freddy Tshimenga kabla ya Humphrey Maseneko kufunga ukurasa wa mabao dakika ya 71. Maseneko alimegewa pasi murwa na Tshimenga.

Nkana inajiandaa kumenyana na Chabab Riadhi Belouizdad ya Algeria katika mechi ya raundi ya kwanza ya mashindano ya Afrika ya Confederations Cup ugenini hapo Machi 6.

Ilikaba mabingwa wa Kenya, Gor Mahia, 1-1 katika mechi ya kirafiki uwanjani Camp Toyoyo mnamo Februari 24, 2018.

Katika mchuano huo, Mrwanda Jacques Tuyisenge alifungia Gor dakika ya 20 kabla ya Nkana kusawazisha kupitia Mbewe dakika ya 64.

Nkana imeratibiwa kuondoka Kenya hapo Februari 27 kuelekea jijini Lusaka kabla ya kupaa hadi jijini Algiers nchini Algeria.

You can share this post!

Ochieng’ hapitiki katika safu ya ulinzi, Mkenya asifiwa...

Usain Bolt aahidi kufichua klabu ya soka aliyojiunga nayo

adminleo