• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Okoth atajwa bora kombe la president Jamal jamal

Okoth atajwa bora kombe la president Jamal jamal

Na CHARLES ONGADI

NAHODHA wa timu ya taifa ya Ndondi Nick Commander’ Okoth amechaguliwa Bondia Bora katika mashindano yaliyomalizika ya President Jamal Boxing Championship katika ukumbi Charter, Nairobi.

Okoth alichaguliwa baada ya kuonesha mchezo wa hali ya juu katika mashindano hayo huku akimnyuka John Mwanzia wa Klabu ya Githurai 44 kwa njia ya knock-out katika fainali ya uzito wa light. Amina Martha wa Klabu ya Kibera Olympics akiibuka bora kwa upande wa akina dada.

Amina aliyekuwa akishiriki mashindano sampuli hii kwa mara ya kwanza, alimduwaza Alice Waiyego wa Nairobi katika fainali ya uzito wa bantam.Aidha, klabu ya Polisi maarufu kama ‘Chafua Chafua’ waliibuka washindi katika mashindano haya kwa kuzoa jumla ya alama 25 wakifuatwa na mahasimu wao wakuu KDF kwa alama 19.

Kibera Olympics ilimaliza ya tatu kwa alama 9 huku Nairobi ikifuata kwa alama 6.Zengine ni Kentrack kwa alama 5, Mombasa na Magereza na zikiwa na alama 3 kila mmoja.Kongowea,Muranga, Githurai 44,Nakuru zote zikipata alama 2. Busia, Kajiado na Thika kila mmoja aliambulia alama moja.

Jumla ya klabu 24 zilishiriki katika Mashindano haya ambayo fainali yake uliohudhuriwa na rais wa Shirikisho la Ndondi Nchini ( BFK) Anthony Otieno Ombok maarufu kama Jamal na mwenyekiti wa Ndondi za malipo nchini Reuben Ndolo.

You can share this post!

Wazalendo yazuru Accra kushiriki mashindano ya hoki Klabu...

Mwatate FC yajipanga kupanda ngazi ligi kuu ya FKF licha ya...

T L