• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 4:36 PM
Ukimwi: Himizo watu waendelee kubaini hali zao

Ukimwi: Himizo watu waendelee kubaini hali zao

NA ALEX KALAMA

BARAZA la Kitaifa la kudhibiti maambukizi ya Ukimwi, limehimiza Wakenya kuendelea kujitokeza kupimwa hali yao.

Akizungumza wakati wa vikao vya kuhamasisha jamii kuhusu kukabiliana na ugonjwa huo, Mshirikishi wa baraza hilo katika eneo bunge la Kilifi Kaskazini, Bw Jacob Kapombe, alisema kuna wengi ambao wamelegeza kanuni za kujilinda dhidi ya maambukizi.

“Kuna wale ambao wanajua wameambukizwa lakini hawaji kuchukua dawa. Lakini kuna wale hata hawajijui kabisa kwa sababu hawajapimwa,” alisema Bw Kapombe.

  • Tags

You can share this post!

Gachagua amtetea Ruto kwa kumteua mgombea mwenza

TAHARIRI: Idara nyingine za serikali ziipe umuhimu lugha ya...

T L