NA ALEX KALAMA
BARAZA la Kitaifa la kudhibiti maambukizi ya Ukimwi, limehimiza Wakenya kuendelea kujitokeza kupimwa hali yao.
Akizungumza wakati wa vikao vya kuhamasisha jamii kuhusu kukabiliana na ugonjwa huo, Mshirikishi wa baraza hilo katika eneo bunge la Kilifi Kaskazini, Bw Jacob Kapombe, alisema kuna wengi ambao wamelegeza kanuni za kujilinda dhidi ya maambukizi.
“Kuna wale ambao wanajua wameambukizwa lakini hawaji kuchukua dawa. Lakini kuna wale hata hawajijui kabisa kwa sababu hawajapimwa,” alisema Bw Kapombe.