• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 1:29 PM
Umeme Bees na mabingwa watetezi Kingstone FC wadenguliwa kwenye hatua ya 16-bora ya Koth Biro

Umeme Bees na mabingwa watetezi Kingstone FC wadenguliwa kwenye hatua ya 16-bora ya Koth Biro

Na CHRIS ADUNGO

MABINGWA watetezi wa Koth Biro Cup, Kingstone FC wamebanduliwa kwenye kampeni za kuwania taji la kivumbi hicho mwaka huu baada ya kupokezwa kichapo cha 2-1 na Leeds United katika mechi ya hatua ya 16-bora iliyochezewa ugani Ziwani, Nairobi mnamo Januari 5, 2020.

Umeme Bees ambao ni wafalme wa zamani wa taji hilo pia walidenguliwa kwenye makala ya mwaka huu kwa mabao 5-3 kutoka kwa limbukeni Ruaraka All Stars. Mshindi wa mechi hiyo aliamuliwa kupitia penalti baada ya pande zote mbili kuambulia sare ya 2-2 mwishoni mwa muda wa kawaida.

Chini ya kocha Issa Winston, Leeds walijiweka kifua mbele kunako dakika ya 18 kupitia kwa Herman Sikubali aliyekamilisha kwa ustadi krosi ya Alex Sunga. Kingstone walisawazisha dakika saba baadaye kupitia kwa Neville Ochieng aliyefunga penalti baada ya Kevin Juma kunawa mpira ndani ya kijisanduku.

Henry Api ndiye aliyefungia Leeds bao la pili na la ushindi katika dakika ya 75.

  • Tags

You can share this post!

Mamelodi Sundowns, Kaizer Chiefs zaingia Klabu Bingwa...

WANGARI: Serikali ibuni mbinu kabambe za kukusanya kodi...