• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 5:55 AM
Familia tajiri hazijadai Sh10.5b zilizoachwa na wapendwa wao – Ripoti

Familia tajiri hazijadai Sh10.5b zilizoachwa na wapendwa wao – Ripoti

Na BERNARDINE MUTANU

Kiwango cha mali ambayo haijadaiwa na wenyewe kimefikia thamani ya Sh10.5 bilioni kulingana na shirika linalosimamia mali hiyo (UFAA).

Kiwango hicho ni kwa muda wa miaka mitatu, kulingana na ripoti iliyowasilishwa Bungeni.

Familia tajiri zina mali ya thamani ya Sh8.53 bilioni katika hazina hiyo. Kulingana na mkurugenzi mkuu wa UFAA Kellen Kariuki, UFAA imeweka masunduku 1,100 ya kuweka salama mali, na ambayo shirika hilo halijui yana mali kiwango kipi kwa sababu hayajafunguliwa.

Shirika hilo pia lina hisa za thamani ya Sh440 milioni ambazo hazijadaiwa na mtu yeyote.

Aina ya mali hiyo ni kama vile pesa zilizoachwa kwa akaunti ambayo haitumiwi tena kwa zaidi ya miaka mitano, hundi za benki ambazo pesa hazikuchukuliwa, na mali ilioko kwa sefu ambazo

  • Tags

You can share this post!

Bei ya stima haitapanda kwa sababu ya ushuru mpya

Harakisheni kuchunguza mauaji ya Sharon – Gavana Obado

adminleo