Habari

Wanajeshi wawili wafariki katika ajali ndege

Na SIAGO CECE June 14th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

MAAFISA wawili wa Jeshi la Anga la Kenya walifariki baada ya ndege kuanguka Jumamosi mchana huko Kinango, Kaunti ya Kwale.

Kamishna wa Kaunti ya Kwale, Stephen Orinde, alithibitisha tukio hilo, akisema maafisa wa usalama bado hawajabaini kama waathirika walikuwa wanafunzi.

Nambari ya usajili ya ndege hiyo ndogo ilikuwa KAF 718.

Chifu wa Eneo la Ndavaya, Naomi Kadama Gofwa alisema wakazi walikuwa wameona ndege mbili zikipita angani katika eneo hilo Jumamosi asubuhi.

‘Nilipata habari saa sita mchana mchana nilipopigiwa simu kwamba chombo hicho kilianguka na watu wawili walikuwa wamejeruhiwa,’ Bi Kadama alisema.

Aliongeza kuwa moja ya ndege zilizokuwa zikizunguka, ghafla ilisimama, ikizunguka mara kadhaa hewani na kuanguka.

Mwezi Machi, ndege ndogo pia kutoka chuo cha mafunzi ya Rubani ( Kenya School of Flying) ilianguka katika eneo jirani la Taita Taveta, mwanafunzi mmoja akiaga.

Ndege hiyo ilitoka Malindi na ilianguka karibu na uwanja wa ndege wa Ikanga huko Voi