• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
MAPISHI: Pasta na mayai

MAPISHI: Pasta na mayai

Na MARGARET MAINA

[email protected]

 

Muda wa kuandaa: Dakika 15

Mapishi: Dakika 20

Walaji: 3

Vinavyohitajika

  • Vitunguu maji 2
  • Mayai 4
  • Pasta
  • Mafuta ya kupikia
  • Chumvi
  • Kitunguu saumu cha unga
Mayai na pasta. Picha / Margaret Maina

 Maelekezo

Injika sufuria yenye maji mekoni kisha weka chumvi ya kutosha.

Weka pasta; hakikisha kwamba hujazikata katikati. Weka ziegemee upande wa sufuria kwani zikipata moto vizuri zitaingia zote kwenye sufuria.

Baada ya dakika 10 pasta zitakuwa zimeiva na kiini kimelainika.

Pasta zikiiva, toa na weka pembeni kwenye sahani.

Menya vitunguu kisha uvikate vipande vidogo. Weka kando.

Bandika kikaango (frying pan) mekoni. Weka mafuta; acha yapate moto kiasi.

Pasua mayai. Ongeza chumvi kisha koroga vizuri.

Weka kitunguu saumu na kitunguu maji kwenye kikaango.

Koroga kiasi na acha kiive kiasi.

Baada ya dakika tatu weka mayai. Tandaza vizuri. Acha yaive upande mmoja, kisha geuza vizuri upande wa pili.

Mayai yakiiva unaweza kutoa na kutenga kwa ajili ya kula.

Pakua chakula chako na ufurahie.

You can share this post!

UKUMBI WA LUGHA: Dhana ya Isimu na Isimu Jamii

Wakulima wa maembe Murang’a walia

adminleo