Kimataifa

Mkuu wa majeshi wa Libya afariki kwenye ajali ya ndege Uturuki

Na MASHIRIKA, WINNIE ONYANDO December 25th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

MKUU wa Majeshi wa Libya na maafisa wengine wanne wa kijeshi wamekufa usiku wa kuamkia leo Desemba 24,2025 baada ya ndege waliyokuwa wakisafiria kuanguka muda mfupi baada ya kutoka mji mkuu wa Uturuki, Ankara.

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki, Ali Yerlikaya amesema mabaki ya ndege hiyo aina ya Falcon 50 yamepatikana kwenye wilaya ya Haymana nje kidogo ya Ankara.

Waziri Mkuu wa Libya Abdulhamid Dbeibah ametuma rambirambi zake akisema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Luteni Jenerali Mohammed al-Haddad.

Mkuu huyo wa majeshi alikuwa nchini Uturuki kwa mazungumzo na viongozi wa ulinzi wa nchi hiyo na mapema hapo jana alikutana na waziri wa ulinzi wa Uturuki Yasar Guler na mkuu wa majeshi ya nchi hiyo.