Onyo kali kwa waume wanaoamka na ‘jogoo’ legevu asubuhi
WATAALAMU wa afya wanaonya kuwa mwanamume anayezinduka usingizini asubuhi jogoo lake likiwa legevu anaweza kuwa na matatizo ya moyo.
Wanaume wengi huamka asubuhi jogoo likiwika, na likilegea inaweza kuwa ishara ya tatizo la moyo.
Kulingana na mtaalamu wa magonjwa ya moyo Dkt Adam C. Powell, kuwika kwa jogoo la mwanamume asubuhi hutokana na mtiririko mzuri wa damu kwenye mishipa ya uume.
“Mtu anapopoteza hii asubuhi, inaweza kuwa ishara ya kuzorota kwa mifumo ya mzunguko wa damu, ambayo ni ishara ya tatizo la moyo,” aliambia Daily Mail.
Hivyo basi, wanaume wanashauriwa kuchukua hatua za mapema, kama vile kupima shinikizo la damu, ili kupunguza hatari ya matatizo ya moyo.