Kimataifa

Iran: Hatutasusia kushiriki Kombe la Dunia ila hatukanyagi Amerika

Na MASHIRIKA March 19th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

TIMU ya Taifa ya Iran imesema inaendelea na mipango ya kujiandaa kwa Kombe la Dunia na haina nia ya kujiondoa kwa kipute hicho hata kama hawataelekea Amerika.

Mkuu wa Shirikisho la Soka Iran Mehdi Taj alisema kuwa hawatajiondoa Kombe la Dunia ingawa alisisitiza hawatacheza Amerika.

“Tutasusia Amerika na hatutasusia Kombe la Dunia,” akasema Taj.

Iran ni kati ya timu ambazo zilikuwa za kwanza kufuzu Kombe la Dunia. Hata hivyo, kushiriki kipute hicho ni hatihati tangu vita vianze kati yao na Amerika mwezi uliopita.

Kombe la Dunia litafanyika kutoka Juni 11 hadi Julai 19 katika nchi tatu — Amerika, Mexico na Canada.

Maarufu kama ‘Team Melli’ wamepangiwa kushiriki mechi zao tatu za makundi Amerika.

Hata hivyo, Taj alisema wanaendelea kushauriana na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) ili mechi hizo zipelekwe Mexico.

Iran itacheza na Nigeria Machi 27 kisha Costa Rica siku nne baadaye kwenye mechi za kirafiki za mataifa manne ambazo sasa watazisakata Jordan kutokana na sababu za kiusalama Ukanda wa Mashariki ya Kati.

“Kikosi cha timu cha taifa kinaendelea na mazoezi Uturuki na kitacheza mechi za kirafiki huki,” akaongeza Taj.