Lugha, Fasihi na Elimu

Suala la malezi na namna linajitokeza katika ‘Nguu za Jadi’

Na JOYCE NEKESA, Kapsabet Boys High School May 6th, 2026 Kusoma ni dakika: 2

LEO tutaangazia baadhi ya maswali likiwemo suala la malezi kwa kurejelea dondoo lifuatalo.

“Wazazi waliasa, ‘Nguo ya kuomba haisitiri makalio.’

Alifunzwa kutotumia sifa za kike alizokirimiwa na Muumba kustarehesha wanaume ili ku jinufaisha kimaisha.

Huku ni kuumbua mwili na tabia. Ali hadharishwa kutomtegemea mume kila wakati ili kumbeba au kuyakimu maisha yake.

Mume huyo akimwondokea, ataanguka mwanguko wa mende. Wala kungwi hakumuusia kuwa na kinywa cha udanganyifu ili apate kitu.

Alielekezwa kutopoteza muda wake kufura hisha walimwengu. Je, ipo haja ya kuifurahisha dunia iliyoshinda ki la juhudi za kuipendeza?”

(a) Eleza muktadha wa dondoo hili
Ni maelezo ya mwandishi. Akimrejelea Mangwasha. Ni wakati Mangwasha alitamani kuwajulisha Waketwa yaliyokuwa yakijiri afisini mwa chifu baada ya kuchomewa makao yao. Ni maelezo kuhusu Mangwasha alivyolelewa na kupewa wosia na wazazi wake.

(b) Fafanua mbinu za mtindo zilizotumika katika dondoo
Methali – Nguo ya kuomba haisitiri makalio.
Nahau – …ataanguka mwanguko wa mende…
Swali balagha – …dunia iliyoshinda kila juhudi za kuipendeza?
Taswira oni – … haisitiri matako.

(c) Suala la malezi limeshughulikiwa kwa kina katika riwaya ya ‘Nguu za Jadi’. Thibitisha
Ngoswe halelewi vizuri. Anadekezwa; anaengwaengwa kupita kiasi. Malezi mabaya yanamfanya kuwa mbadhirifu wa mali ya umma. (Uk.122)

Wazazi hawawajibiki. Sihaba anakubaliana na baadhi ya akina mama wanaomletea wasichana wao Red Bead Lodgings (RBL) ili walipwe (Uk.143)

Umasikini unawafanya baadhi ya wazazi kushindwa kutimiza mahitaji ya kimsingi ya wanao; vigoli wengine wanatorokea RBL kwa kukosa lishe nyumbani.

Ulevi unamzuia Mrima kuwa mlezi mwema. Haelimishi wala kulisha wanawe hadi watoto wanamsahau.

Wazazi wana wajibu wa kuwashauri wana wao; kwa mfano, Mangwasha aliusiwa kuambaa uvivu.

Wosia unaompa mwongozo wa kukabiliana na maisha. Malezi mema huwaandaa watoto kwa ugumu wa maisha katika siku za baadaye.

Mangwasha alitahadharishwa kuwa dunia hupiga watu vikumbo, huwachenga na kuwaghilibu wakakosa pa kutia uso. (Uk.12)

Mangwasha anausiwa asitumie udanganyifu ili kupata kitu. (Uk.12)

Mangwasha anakuwa mlezi mwema kwa Sayore na Kajewa alipotelekezwa na mumewe.

Watoto wa mtaani Ponda Mali walikosa malezi mema, hawakuenda shuleni, walivaa mararu na kuokota vipande vya sigara na kuvivuta. (Uk.34)

Wasichana wadogo walitwika jukumu la ulezi wa mapema na kuishia kuwa majeruhi wa jamii. (Uk.137-138)

Wazazi wa kiume wana kadhia nyingi wanazojishughulisha nazo na hawana wasaa wa kuwafundis ha watoto wavulana lolote la maana.