Habari

Nyoro apendekeza mbinu ya kushusha bei ya petroli nchini

Na MOSES NYAMORI May 16th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MBUNGE wa Kiharu, Ndindi Nyoro ameanzisha mapendekezo mawili ya marekebisho ya sheria yanayolenga kupunguza bei ya mafuta kwa zaidi ya Sh26 kwa lita.
Bw Nyoro ambaye alikuwa mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Bunge ameandikia Karani wa Bunge la Kitaifa Samwel Njoroge kuhusu nia yake ya kuwasilisha marekebisho ya Sheria ya Ushuru wa Thamani (VAT).
Mbunge huyo anapendekeza bidhaa za petroli ziondolewe ushuru wa VAT.
Katika pendekezo jingine, mbunge huyo anataka ushuru wa Hazina ya Ukarabati wa Barabara (RMLF) upunguzwe kwa Sh7 ili ushuru wa sasa wa Sh25 kwa lita ushuke hadi Sh18.
Bw Nyoro pia aliitaka serikali kutoa Sh5 bilioni kutoka Hazina ya Kudhibiti Bei ya Mafuta ili kuwakinga Wakenya dhidi ya ongezeko la bei ya dizeli ambalo alisema linaweza kulemaza uchumi wa taifa. “Dizeli ina gharama kubwa zaidi ya uagizaji. Ni lazima tutenge Sh5 bilioni kutoka Hazina ya Kudhibiti Bei ya Mafuta,” alisema.