Habari za Kaunti

Godhana alalamika Mungatana hampi nafasi kukamilisha muhula wake kwa amani

Na WINNIE ATIENO May 19th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

KITI cha useneta katika Kaunti ya Tana River 2027 kinazidi kuibua joto la kisiasa, huku Seneta Danson Mungatana, akiendelea kukosoa utawala wa Gavana Dhadho Godhana.

Hivi majuzi, Bw Godhana ambaye anatarajiwa kuwania useneta baada ya kustaafu ugavana mwaka ujao, alimkashifu Bw Mungatana kwa kuingilia kazi yake.

Akizungumza wakati w kuchangisha fedha katika kanisa la AIC Bura Tana wikendi, Bw Mungatana alidai bajeti ya kaunti inalenga zaidi matumizi ya afisi ya Gavana kuliko miradi ya maendeleo.

Bw Mungatana aliwataka wananchi kuchagua viongozi wenye mipango ya maendeleo na kuwahimiza kushiriki kikamilifu katika uchaguzi ujao, ili kuchagua viongozi wanaoleta maendeleo badala ya siasa.

Alisema anaendelea kupigania ongezeko la mgao sawa wa fedha za kaunti lakini ni wajibu wa serikali ya kaunti kuzitumia vyema.