Kimataifa

Hofu joto kali likiua watu 1,000

Na MASHIRIKA June 28th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

UFARANSA imerekodi vifo vya ziada 1,000 katika msimu wa joto kali lililogubika Uropa, idara ya afya umma ilisema jana, ikionya kuwa idadi halisi huenda ni ya juu zaidi.
Ikielezea kwa kina idadi ya mwanzo kuhusu vifo, Sante Publique ilisema sehemu kubwa ya vifo ilihusu watu wazee na kwamba inatarajia vifo kuongezeka huku habari zaidi zakijitokeza kuhusu vifo katika makazi na nyumba za wazee Raia wa Uropa wamestahimili hali ya anga yenye joto kali kwenye mawimbi ambayo yamehusishwa na vifo vya watu kadhaa – kuvunja rekodi, kuvuruga uzalishaji nishati na kuharibu miundomsingi.
Wanasayansi wamesema mawimbi ya joto, yaliyoanza Juni 20, ni mabaya zaidi kuwahi kurekodiwa Uropa, ambapo hali ya anga inabadilika kwa kasi zaidi kuliko kiwango cha jumla duniani.
Mawimbi ya joto yanaelekea Mashariki. Lakini huku idara ya hali ya anga Ufaransa ikisema joto kali kupindukia limepungua katika sehemu nyingi nchini, baadhi ya maeneo Kaskazini Mashariki bado yalikuwa chini ya ilani kali.
Waziri wa Afya, Stephanie Rist alieleza gazeti linalofahamika kama La Tribune kwamba athari za mawimbi ya joto kali huenda zikaendelea kwa muda wa siku 10 zaidi baada ya hali ya anga kutulia.