Kidosho ashangaza pasta wake kukiri hataenda krusedi sababu hajaokoka kikamilifu
KIDOSHO alimwacha pasta wake katika mshangao alipokiri kwamba ataangusha injili iwapo ataandamana naye katika krusedi ya nyumba kwa nyumba, eti kwa sababu tabia zake zingaliwa za kutiliwa shaka.
Duru zinaarifu kuwa kipusa huyo ni mshiriki wa kanisa la hapa na mara kadha pasta humtegemea na kumwamini sana katika masuala ya imani.
Hivi majuzi mchungaji aliamua kupiga injili katika kijiji cha kipusa huyo na kumtaka aandamane naye.
Mara moja kipusa akamjibu mtumishi kwamba atafute mtu mwingine huku akiungama kwamba ripoti zake kijijini ni mbaya sana.
“Acha niseme ukweli. Kwa kondoo wenzangu kanisani mimi ni mlokole kamili, lakini nyumbani mambo ni tofauti kabisa. Ninajulikana kwa matendo yasiyotajika, ila hivi karibuni nitayaach,” mrembo alikiri mbele ya mchungaji huku akiona haya kuu.