• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 6:50 PM
Mpasuko zaidi Jubilee wabunge wakikabana koo

Mpasuko zaidi Jubilee wabunge wakikabana koo

JOSEPH Beginner bodybuilding program: the coach’s exercises for training at home stanozolol reviews the zone – fitness, bodybuilding and nutrition myprotein. WANGUI na WYCLIFFE MUIA

MPASUKO katika chama cha Jubilee unaendelea kupanuka huku wabunge wa chama hicho tawala wakiendelea kurushiana cheche za maneno kuhusiana na vita dhidi ya ufisadi.

Siku chache baada ya wabunge wa Jubilee kutoka Rift Valley kumshambulia Rais Uhuru Kenyatta kwa madai ya kumhujumu naibu wake William Ruto, wenzao wa Kati wamejitokeza kutetea msimamo wa Rais kuhusu vita dhidi ya ufisadi.

Wabunge hao Rahim Dawood (Imenti Kaskazini), Muturi Kigano (Kangema) na Maina Kamanda (maalum), wamewakashifu wenzao wa Rift Valley kwa kuingiza siasa katika juhudi za kupambana na ufisadi nchini.

Viongozi hao wa Kati walimtaka Seneta wa Elgeyo Marakwet Kipchumba Murkomen na Mbunge wa Kapseret Oscar Sudi kukoma kumshambulia Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai (DCI) George Kinoti.

“Murkomen na Sudi wanapaswa kukoma kumshambulia DCI. Kwa nini wanapiga kelele hata kabla ya uchunguzi kukamilishwa?,”alishangaa Bw Kamanda.

Bw Kamanda alidai baadhi ya viongozi wa Rift Valley wanataka kutibua uchunguzi wa mabwawa ya Arror na Kimwarer kwa sababu wanahusika katika sakata hiyo.

“Kuna hofu kuwa ukweli utafichuliwa hivi karibuni na wale ambao hawana hatia hawapaswi kutetemeka,”aliongeza Bw Kamanda.

Naye Bw Dawood aliwasuta baadhi ya wabunge wa Rift Valley kwa kulemaza juhudi za kupambana na ufisadi na kutaka Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) pamoja na maafisa wa DCI wasitishwe na yeyote.

Haya yanajiri siku chache baada ya mbunge wa Gatundu Kusini, Moses Kuria kudai kuwa chama cha Jubilee kimevunjika tayari.

Siku chache zilizopita, Murkomen na Sudi waliongoza wabunge wa Rift Valley kuwakashifu maafisa wa DCI na DPP kwa madai ya kugeuza vita dhidi ya ufisadi kumhujumu Naibu Rais katika siasa za 2022.

Hata hivyo, Gavana wa Elgeyo Marakwet Alex Tolgos Jumatatu alitofautiana na wenzake kuhusu vita dhidi ya ufisadi na kumuomba radhi Rais kuhusiana na matamshi makali yaliyotolewa mwishoni mwa juma na baadhi ya wenzake kuhusu uchunguzi unaoendelea wa sakata ya ujenzi wa mabwawa mawili katika kaunti yake.

Wiki iliyopita, baadhi ya wabunge walitishia kuongoza maandamano dhidi ya serikali ikiwa Rais Kenyatta atathubutu kusitisha ujenzi wa mabwawa ya Arror na Kimwarer kwa sababu ya madai ya wizi wa Sh21 bilioni za kufadhili miradi hiyo.

Wakiongozwa na Daniel Rono (Keiyo Kusini), Kangogo Bowen (Marakwet Mashariki), William Kisang (Marakwet Magharibi) wabunge hao walisema wako tayari kuanzisha uasi dhidi ya utawala wa Rais Kenyatta ikiwa miradi hiyo itasimamishwa kwa sababu ya uchunguzi unaoendelea kuhusu sakata hiyo.

Spika wa bunge la Elgeyo Marakwet, Bw Philemon Sabulei alisema madai ya ufisadi yanayoelekezwa katika mabwawa ya Kimwerer na Arror yanaongozwa na siasa za ubinafsi wala si vita dhidi ya ufisadi.

Bw Sabulei alidai kuwa vita hivyo vinalenga kuzima azma ya naibu kuelekea Ikulu 2022.

Viongozi hao waliapa iwapo waziri wa fedha Henry Rotich ataachishwa kazi kama ilivyokuwa kwa waziri wa michezo Rashid Achesa, jamii ya Wakalenji haitakuwa na budi ila kujitoa katika muungano wa Jubilee na kutafuta mbinu nyingine ya kumwezesha Naibu Rais kutwaa uongozi wa nchi 2022.

You can share this post!

NGILA: Teknolojia inayoua wanadamu yafaa kukomeshwa

Sikumfuta kazi Matiang’i, asema Magoha

adminleo