• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 2:56 PM
Nyumba 50 zateketea Mukuru-Kaiyaba

Nyumba 50 zateketea Mukuru-Kaiyaba

Na SAMMY KIMATU

ZAIDI ya watu 100 walikesha nje penye baridi baada ya nyumba 50 kuteketea katika eneo la Dallas kwenye mtaa wa mabanda wa Mukuru-Kaiyaba mwishoni mwa juma.

Moto huo ulianza katika nyumba moja baada ya vijana wawili kuzozana na kisha ukachochewa na upepo mkali.

Gari mbili za kuzima moto kutoka Kuanti ya Nairobi fauka ya kuwasili mtaani hazikufaulu kufika kwenye eneo la mkasa kufuatia ukosefu wa njia baada ya barabara kunyakuliwa.

Watoto watazama wasijue la kufanya baada ya nyumba zao kuchomeka. Picha/ Sammy Kimatu

Bi Monicah Juma, 43, ambaye kadhalika ni mhuduu jamii wa kujitolea alisema aliarifiwa kuhusu mkasa huo na mtoto lakini alipowasili akakuta nyumba yake imeteketea. Hakuokoa chochote.

Bw Onesmus Kalei, mkazi m,taani humo na mmiliki wa nyumba kwenye eneo la kisa alisema vijana walipigana kwa ukucha na jino wakitumia maji ya mifereji huku wengine wakibomoa nyumba moto usienee Zaidi.

Aliwaomba wakazi kubomoa vibanda na nyumba ikiwa watanusuru maisha yao na mali ndiposa njia ya dharura ipatikane.

Wanaume wakusanya mabati ya nyumba zao zilizochomeka. Picha/ SDammy Kimatu

Huku shule zikiwa zimefungwa, nao watoto walifurika kutafuta vyuma kuukuu na vingine vya dhamana kwao.

“Huu mkasa ni wa saba kutokea mtaani huo mwaka huu pekee,” Bw Kalei akaambia wanahabari.

You can share this post!

Tabichi ateuliwa balozi wa kuwatetea watoto duniani

Kenya yapoteza mataji ya wanaume na wanawake Paris Marathon

adminleo