• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 6:55 AM
VIDUBWASHA: Inatumia laini mbili za simu (Infinix S4)

VIDUBWASHA: Inatumia laini mbili za simu (Infinix S4)

Na LEONARD ONYANGO

KAMPUNI ya Infinix ya Hong Kong imezindua simu mpya ya Infinix S4 ambayo huenda ikawa kivutio kwa wapenzi wa picha za selfie.

Infinix S4 ina kamera nne, tatu nyuma na moja ya selfie.

Kamera ya selfie ni ya 32MP na hiyo inamaanisha kwamba inanasa picha za ubora wa juu.

Kamera za nyuma ni 13MP, 8MP na 2MP.

Ina betri ya 4,000Ah ambayo kampuni hiyo inadai kwamba inaweza kutumika kwa siku mbili kabla ya kuchajiwa.

Inatumia laini mbili za simu na inaweza kuhifadhi data ya ukubwa wa 32GB bila kuongezewa kadi sakima (memory card).
Inaweza kufunguliwa kwa alama za vidole au uso.

You can share this post!

Kisumu All Stars waweka hai tumaini la kutinga KPL baada ya...

Rais nisamehe, watu wananidharau sasa, Echesa alia

adminleo