• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 11:05 AM
Joyce Akinyi akamatwa tena kuhusu mihadarati

Joyce Akinyi akamatwa tena kuhusu mihadarati

Na Benson Matheka

MFANYABIASHARA mbishi wa Nairobi, Joyce Akinyi na mwanamume raia wa Congo, walikamatwa jana kwa kushukiwa kulangua dawa za kulevya.

Polisi walisema kwamba walivamia chumba ambacho Akinyi na mwanamume huyo walikuwa wakiishi katika mkahawa wake wa Deep West jijini Nairobi na kupata kilo 2 za heroin ya thamani ya Sh3 milioni.

Inasemekana kuwa Akinyi anayekabiliwa na shtaka la kulangua dawa za kulevya katika mahakama ya Kibera alikuwa na paspoti iliyoonyesha ni raia wa Congo.

Wapelelezi wanashuku kwamba alikuwa akitumia paspoti hiyo kuzuru mataifa tofauti nchini kuendeleza biashara ya mihandarati.

Wawili hao wanazuiliwa katika kituo cha polisi cha Muthaiga wakisubiri kufunguliwa mashtaka.

Hii ni mara ya tatu kwa Akinyi kukamatwa kwa kushukiwa kuhusika na biashara ya dawa za kulevya.

Mnamo 2015 alikamatwa pamoja na watu wengine watatu na kushtakiwa katika kesi inayoendelea katika mahakama ya Kibera.

 

You can share this post!

Ajabu ya matajiri wa mahindi kumezwa na ufukara

‘Team Wanjiku’ wapeleka kampeni Mombasa

adminleo