• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 9:50 AM
Demu aangua kilio alipokosa wa kumnunulia bia

Demu aangua kilio alipokosa wa kumnunulia bia

Na JOHN MUSYOKI

EMBU MJINI

DEMU mmoja mjini hapa aliangua kilio wanaume walipokataa kumrushia mistari ya mapenzi na kumnunulia pombe.

Duru zinasema demu alifika kilabuni mwendo wa saa kumi na moja wanaume walipokuwa wakijaajaa kujiburudisha. Alisimama karibu na mlango kwa dakika kadhaa kisha akaingia ndani na alipoulizwa na wahudumu alichotaka kuuziwa hakusema chochote.

Kulingana na mdokezi, mwanadada huyo aliwakodolea macho wanaume waliokuwa wakiingia kilabuni na wengine wakiendelea kuteremsha dozi.

Mhudumu wa kilabu hicho alienda kumsalimia lakini demu akampuuza. “Nikusaidie vipi? Itisha unachotaka, hapa tunaruhusu wateja peke yake,” mhudumu huyo alisikika akimwambia demu. Inasemekana demu alikataa katakata kuondoka alikokuwa ameketi karibu na mlango.

“Sitaki kuongea na wewe. Mwanamke kama mimi utanisaidia na nini? Nashangaa sana. Kwani wanaume hawa wa huku kwenu ni wa aina gani, hata hawataki kunitongoza.

“Mimi ni mrembo lakini wanaume wa huku ni wachoyo sana,” demu alimwambia mhudumu huku akidondokwa na machozi.

“Sasa unalia kwa nini. Ni nani amekukosea hapa kilabuni? Kwenu ni wapi na unafanya kazi gani,” jamaa mmoja alimuuliza demu alipomuona akilia.

Hata hivyo baadhi ya wanaume walimkashifu mwanadada huyo. “Aondoke hapa kilabuni. Demu huyo hana nia nzuri na huenda ni tapeli.

“Mwambie wateja wa kilabu hiki ni wachoyo kwa machangudoa. Wanawake wa siku hizi wanapenda kuvuna wasikopanda,” jamaa mmoja alisikika akisema.

Inasemekana demu alianza kuzusha lakini akaondolewa juu juu na wahudumu wa kilabu hicho huku wakimfokea vikali. Ilibidi demu kuondoka huku akiangua kilio lakini hakuna mtu aliyemjali.

You can share this post!

Mganga wa TZ anayedai kufufua maiti akamatwa Taveta

MAZINGIRA NA SAYANSI: Je, washangaa kwa nini mende...

adminleo