• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 5:55 AM
MAPISHI: Jinsi ya kuoka biskuti iliyoongezwa chokoleti

MAPISHI: Jinsi ya kuoka biskuti iliyoongezwa chokoleti

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 15

Muda wa kupika: Dakika 15

Walaji: 5

Vinavyohitajika

  • Vikombe 3 vya unga wa ngano
  • Kijiko 1 cha baking soda
  • Kijiko 1 cha chumvi
  • Kikombe ¾ ya siagi iliyoyeyuka
  • Kikombe ½ ya sukari nyeupe
  • Kikombe 1 cha sukari ya brown
  • Vijiko 2 vya vanilla extract
  • Mayai 2
  • Vikombe 2 vya chocolate chips

Maelekezo

Kwenye bakuli kubwa, changanya unga wa ngano, chumvi na baking soda.

Changanya unga wa ngano, chumvi na baking soda. Picha/ Margaret Maina

Kwenye bakuli jingine kubwa, changanya sukari nyeupe, siagi, mayai na vanilla mpaka mchanganyiko ulainike vizuri.

Changanya mchanganyiko wa unga na mchanganyiko wa sukari kisha ukande mpaka uchanganyike vizuri kabisa.

Changanya mchanganyiko wa unga na mchanganyiko wa sukari kisha ukande. Picha/ Margaret Maina

Ongeza chocolate chips. Changanya vizuri kisha funika bakuli. Acha unga ulale kwenye jokofu usiku kucha.

Gawanya mchanganyiko wa unga kwa kipimo cha vijiko vitatu vya chakula. Tengeneza mduara kama vijipira. Panga vizuri kwenye chombo cha kuokea ukitumia karatasi za kuokea.

Oka kwenye ovena iliyopata moto katika joto la nyuzi 175 sentigredi kwa robo saa au mpaka zianze kupata rangi ya kahawia.

Epua, acha zipoe kabla ya kuhamishia kwenye waya wa kupozea zipoe kabisa.

Pakua na ufurahie.

You can share this post!

Manchester United yazidi kukaa ngumu kuhusu Pogba

Matiang’i atabomoa mafia wa mihadarati?

adminleo