• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:55 AM
Viongozi wa kidini: Weta na Mudavadi wakomeshe siasa za ukabila

Viongozi wa kidini: Weta na Mudavadi wakomeshe siasa za ukabila

Na JUSTUS OCHIENG’

VIONGOZI wa dini eneo la Nyanza wamewalaumu vinara wawili wa Nasa- Musalia Mudavadi na Moses Wetenga’ula kwa kuendeleza siasa za ukabila kumlenga kiongozi muungano huo wa Nasa Raila Odinga katika eneo la magharibi.

Wahubiri hao wa baraza la viongozi wa kanisa waliwashutumu Mudavadi na Wetang’ula kwa kuendeleza kampeini za mgawanyiko na uchochezi dhidi ya Bw Odinga.

“Tunamtaka Bw Wetang’ula aendeleze kampeni zinazolenga kuwaunganisha wakenya. Hii ni kwasababu nchi hii inahitaji kuletwa pamoja baada ya siasa za migawanyiko na chuki kutokana na kampeni za mwaka uliopita,” kiongozi wa baraza hilo Askofu Washington Ongonyo-Ngede alisema.

Mnamo Jumamosi, Mabw Mudavadi na Wetang’ula waliambia jamii ya Walhuya wamkatae Bw Odinga na kumlaumu “kwa kuitumia jamii hiyo na kuitema.”

Shambulizi hili dhidi ya Bw Odinga linatokana na kung’atuliwa kwa Bw Wetang’ula kutoka wadhifa wake wa kiongozi wa walio wachache katika bunge la Seneti.

Wadhifa huo umetunukiwa Seneta wa Siasa James Orengo.

Lakini jana viongozi wa dini kutoka Nyanza wakiongozwa na Askofu Ngede walimtahadharisha dhidi ya madai kwamba ataimbua kampeini za kumpinga Bw Odinga.

Katika taarifa iliyotiwa saini na maaskofu saba Ogonyo-Ngede, Julius Otieno, Dkt Hesbon Omwandho Njera, Habakuk Abogno, Dkt William Abuka, Geoffrey Owiti na Rev Job Othatcher viongozi walimtakaka Bw Wetang’ula akome “mara moja kuendeleza kampeni za mgawanyiko na badala yake aanze mikakati ya kuwaunganisha wananchi kwa minajili ya maendeleo.”

Maaskofu hao waliwashauri wakenya wakumbatie uhusiano uliozinduliwa na Rais Uhuru Kenyatta na Bw Odinga kuimarisha nchi hii.

Wahubiri hao walisema Bw Odinga yuko huru kushauriana na Rais Kenyatta kutafuta namna ya kuleta uuwiano nchini.

“Seneta Wetang’ula anapasa kujua aliyekuwa waziri mkuu ni kiongozi wa kitaifa anayeongoza watu na wala sio wananchi wanaomwongoza,” alisema Askofu Ngede.

You can share this post!

Kizaazaa Miguna kuzuiwa JKIA akitoka Canada

Maafisa ndani kwa kumeza hela za makaburi

adminleo