• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 6:50 AM
Hospitali ambako wagonjwa wanafariki ziadhibiwe – Mahakama

Hospitali ambako wagonjwa wanafariki ziadhibiwe – Mahakama

Na RICHARD MUNGUTI

JAJI mmoja katika Mahakama Kuu amesema kwamba hospitali ambako wagonjwa wanafariki zinapaswa kuadhibiwa kwa kutokuwa na makini.

Jaji Roselyn Aburili alimwagiza mwanasheria mkuu , Tume ya kufanyia Marekebisho Sheria na Wizara ya Afya kufanyia marekebisho sheria ya bodi ya madaktari kwa lengo la kuzuia wagonjwa kufa ovyo ovyo kwa kupuuzwa.

Jaji Aburili alisema madaktari wengi wamekuwa na tabia ya kutojali . Alisema madaktari kama hawa wanapasa kuadhibiwa vikali kwa vile wanakaidi sheria ya kuwajali wagonjwa.

“Wagonjwa wengi wamepoteza maisha yao wakiwa mahospitali wanakopaswa kusaidika,” alisema Jaji Aburili.

Jaji huyo alisema hayo alipoamua kesi iliyowasiolishwa na jamii ya wakili aliyefia hospitalini katika sababu ambazo haziueleweka.

Katika kesi hiyo iliwasilishwa na Chama cha Hospitali nchini (KHA) na hospitali ya Nairobi zilizoshtaki bodi ya madaktari KMDB baada ya bintiye Bw John Paul Odero,  Sybil Masinde Odero kufia katika hospitali.

Sybil aliaga Feburuari 11, 2011 akiwa chini ya uangalizi wa Dkt Bartilol Kigen. Sybil alifanyiwa upasuaji akijifungua kisha akafariki baada ya muda mfupi.

Jaji Aburili aliamuru waliohusika wachukuliwa hatua kali.

You can share this post!

Sonko akubaliwa kuwafurusha wanabodaboda kutoka katikati ya...

Biashara haramu ya makaa inayowafaidi Al-Shabaab msituni...

adminleo