• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 6:50 PM
Kujiondoa kwa Sportpesa na Betin kutaisaidia nchi pakuu – Kanini Kega

Kujiondoa kwa Sportpesa na Betin kutaisaidia nchi pakuu – Kanini Kega

Na Stephen Munyiri

MBUNGE wa Kieni Bw Kanini Keega ameunga mkono hatua ya kampuni za kamari za Sportpesa na Betin kusimamisha shughuli zake nchini.

Mbunge huyo, ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati ya Bunge kuhusu Biashara, alisema kuwa uchezaji kamari umewaathiri sana vijana wengi na kuwafanya wazembee katika utafutaji pato.

Bw Kega alisema kwamba ijapokuwa serikali huwa inawaunga mkono wawekezaji wa kigeni, mchipuko wa kampuni za kucheza kamari haukuzi uchumi wa nchi.

Alisema kuwa kampuni hizo hazikuchangia lolote kuwawezesha Wakenya kujikuza kiuchumi.

“Kama serikali, tunaunga mkono kampuni ambazo zitawezesha Wakenya kujikuza kiuchumi. Hata hivyo, baadhi ya wawekezaji kama wale wanaojihusisha kwenye biashara ya uchezaji kamari hawachangii lolote,” akema mbunge huyo.

Alisema hayo kwenye kikao na wanahabari katika Kanisa la PCEA Kabiru-ini wakati wa kutawazwa kwa Kaasisi Peter Maikumi mnamo Jumapili.

 

You can share this post!

Ni vilio tupu katika ndoa ya Uhuru na Joho

Wito vituo vya intaneti vianzishwe mashinani

adminleo