• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 3:03 PM
Iweje Kenya impeleke Miguna Dubai akateseke kama yatima? auliza Makau Mutua

Iweje Kenya impeleke Miguna Dubai akateseke kama yatima? auliza Makau Mutua

Mfanyabiashara maarufu Jimi Wanjigi (kushoto), wakili Prof Makau Mutua, Bw Raila Odinga na watu wengine wakiwa katika kesi ya Miguna Miguna Machi 29, 2018. Picha/ Richard Munguti

Na RICHARD MUNGUTI

WAKILI mwenye tajriba ya juu anayeishi Marekani Profesa Makau Mutua, kinara wa Nasa Raila Odinga na mamia ya mawakili walihudhuria kesi ya kuadhibiwa kwa waziri wa usalama Fred Matiang’i, mkurugenzi wa Idara ya Uhamiaji meja mstaafu Gordon Kihalangwa na Mkuu wa Polisi  Joseph Boinnet kwa kumfurusha wakili mbishi Miguna Miguna na Jaji George Odunga Alhamisi.

Prof Makau alisema ni ukiukaji mbaya wa haki za binadamu kwa raia kusafirishwa kutoka nchi yake na “kupelekwa nchi ya ng’ambo kuteseka kama yatima.”

Wakili James Orengo anayemwakilisha Miguna aliomba Jaji Odunga akiomba korti iwasukume jela Matiang’i, Kihalangwa na Boinnet miaka mitatu jela alisema , “nchi ya Canada iko afadhali mara mia kuliko Kenya kwamba sababu inamtunza Miguna ilhali nchi ya Kenya inamtesa.”

Bw Orengo alimrai Jaji Odunga akisema , “Jamaa hawa Boinnet, Kihalangwa na Matiang’i wanapasa kuanza kuenda gereza kuu la Kamiti huko watapewa makao bora sio choo kama vile walimweka wakili wa kimataifa mwenye tajriba ya juu Dkt Miguna.”

Bw Orengo alisema wakuu hao watatu wanaidharau mahakama sana na “korti yapasa kujitetea dhidi ya wakaidi kama hawa.”

Bw Orengo alisema ni jambo la kusikitisha sana kwa maafisa wa usalama kumdunga dawa apoteze ufahamu na kumsafirisha Dkt Miguna.

Bw Odinga hakukaa sana kortini na wala hakuhutubia wanahabari.

You can share this post!

Orengo ataka Miguna aundiwe pasi maalum ya usafiri...

Jombi atisha kutimua mke kwa kukataa kuamini ushirikina

adminleo