• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 6:55 AM
Mwanamume aliyejifanya Sabina Chege na kuwatapeli wabunge anaswa Tanzania

Mwanamume aliyejifanya Sabina Chege na kuwatapeli wabunge anaswa Tanzania

Na CHARLES WASONGA

MWANAMUME anayehutumiwa kuwadhulumu wabunge mitandaoni na kuwapunja hela hatimaye ametiwa mbaroni na anazuiwa katika kituo cha polisi cha Muthaiga, Nairobi.

Benson Wazir Chacha (pichani kushoto) aliletwa na polisi hadi Nairobi Jumatatu baada ya kukamatwa katika hoteli moja mjini Tarime, nchini Tanzania Jumapili.

Ilidaiwa kuwa mshukiwa huyo alikuwa amejificha huko baada ya kusakwa na polisi kwa muda wa wiki moja maovu yake yalipofichuliwa na Mbunge Mwakilishi wa Wanawake, Bi Sabina Chege.

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai (DCI) George Kinote alisema mshukiwa atafikishwa mahakamani Jumanne kujibu mashtaka kadhaa.

Bw Chacha anatuhumiwa kuitisha pesa kutoka kwa wabunge kwa kisingizio kuwa alikuwa Bi Chege na alikuwa katika hali “mbaya zaidi ambapo alihitaji wenzake kumnusuru”.

Bw Kinoti alisema mshukiwa alikuwa anapanga kutorokea taifa la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Mkurugenzi huyo wa upelelezi alifichua kuwa mshukiwa alinaswa kutokana na usaidizi kutoka polisi wa Tanzania walioshirikisha msako huo na kisha kusaidia kumsafirisha hadi mji wa mpakani wa Isebania.

Vile vile, Shirika la Polisi wa Kimataifa (Interpol) limekuwa likishirikiana na maafisa wa usalama wa Kenya na Tanzania  katika juhudi za kumsaka Bw Chacha.

 “Kikosi changu nilichobuni wiki moja iliyopita kimekuwa kikipanga na kukusanya habari ambazo zilisaidia katika kutiwa mbaroni kwa mshukiwa,” Bw Kinoti akasema.
Wiki iliyopita mkuu huyo wa DCI alitoa wito kwa umma kusaidia katika kutoa habari zitakazosaidia wapelelezi kumkamata Bw Chacha na akatoa zawadi ya Sh20,000.
Washirika wake watatu, akiwemo ajenti wa M-Pesa pia wameshikwa.

Ajenti huyo, kulingana na wapelelezi, alishirikiana na walaghai kusajili akaunti ya M-Pesa kwa jina na maelezo ya Bi Chege.

Baadhi ya maafisa wa serikali ambao wamepunjwa na Bw Chacha ni Spika wa Bunge la Kitaifa Justin Muturi (Sh300,000), aliyekuwa Mbunge wa Gem Jakoyo Midiwo (Sh20,000), mawaziri Eugene Wamalwa (Ugatuzi), Peter Munya (Afrika Mashariki), Profesa Margaret Kobia (Utumishi wa Umma) na Bi Sicily Kariuki.

You can share this post!

Sitakubali tena kuwa mgombea mwenza – Kalonzo

Wa Muchomba atawataka wanaume kuoa wake wengi

adminleo