• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 5:39 PM
SHANGAZI: Kila niendapo kwa duka lake, hulalama kuhusu mumewe

SHANGAZI: Kila niendapo kwa duka lake, hulalama kuhusu mumewe

Mimi ni kijana na nilioa miaka mitatu iliyopita. Nina mtoto mmoja. Tatizo ni kwamba, kuna mwanamke mwenye biashara ya nguo. Niendapo kununua wakati ninapotoka, yeye huniandama na kunilalamikia kuhusu mume wake. Nifanyaje?
Kupitia SMS

Watu hulemewa na matatizo na huwa wanatafuta jinsi ya kutua mzigo wa mawazo na hofu. Hivyo labda huyu dada ameona unaweza kumsikiliza na kumsaidia kutua aliyo nayo. Hata hivyo ni muhimu kuwa mwangalifu ili usijipate umetekwa kimapenzi. Ni vizuri kufafanua kwake kwamba nia yako ni kumsikiliza na labda kumpa usaidizi wa kupata suluhu na wala sio vinginevyo.

 

Natafuta mke wa mtu
Naitwa Maguta kutoka Narok. Nina mke na watoto wawili. Natafuta wanawake wanene na pia wake za watu. Aliye tayari ajitokeze. Kupitia SMS

Nadhani unatamani kupigwa, ama umechoka kuishi.

 

Nashuku nina mimba
Mimi ni msichana wa umri wa miaka 24. Nina mume ambaye nikilala naye natokwa na maji na nina mimba ya miezi sita. Niko Mombasa. Kupitia SMS

Unapokuwa mjamzito ni muhimu mno kuwa makini na kinachoendelea mwilini mwako hasa inapohusu burudani. Siwezi kujua kwa uhakika kama hali hiyo ni kawaida ama la. Bali itakuwa vyema umuone daktari,akuangalie na akupatie jibu la kitaalamu. Kwa sasa pumzisha burudani na mumeo hadi utakapomuona daktari.

 

Namtafuta kidosho
Mimi ni kijana wa umri wa miaka 25. Natafuta mpenzi. Awe anajiweza na umri wa miaka 30. Awe Muislam hasa Muarabu. Kama uko jitokeze.
Mohamed. Mombasa. Kupitia SMS

Natumaini unayemtafuta atajitokeza.

 

Ninachukia wanaume
Nina umri wa miaka 19. Sina mpenzi na wanaume watatu wananiandama. Nawachukia wanaume. Je, hii ni sababu ya kukosa mpenzi? Nifanyaje waache kunifuata? Kupitia SMS

Inawezekana pia umri wako unachangia pakubwa hiyo chuki uliyo nayo kwa wanaume. Ingawa pia inaweza kuwa mambo yaliyokutokea wakati unakua ama yale ambayo uliyashuhudia kuhusiana na wanaume. Jipatie wakati ukue, ukomae zaidi.

 

Kuna dawa ya chuma?
Chuma changu ni nchi nne unusu. Je, ni kidogo? Na kuna dawa? Kama ipo inaitwaje? Niipate wapi? Hussein Ali. Umri wangu ni miaka 24.
Kupitia SMS

Haya maswali yako ni kama ya afisa wa upelelezi. Huna haja ya kujiuliza haya yote, bali unatakiwa kulenga mbinu na jinsi za kutumia ulicho nacho kumfurahisha mwenzako. Kwani raha ya mapenzi sio ukubwa wa chuma, bali mbinu za kukitumia.

 

Niko tayari kumwoa
Nina umri wa miaka 20. Jina langu ni Bihija. Niko tayari kuishi na Twaha. Kupitia SMS

Natarajia huyo mwenzako amesikia mwitikio wako.

 

Nampenda lakini hajui
Naitwa James kutoka Thika. Kuna mrembo ninayempenda sana lakini sijamwambia. Kwani yuko sekondari na nataka kumpa muda amalize. Lakini naogopa atapatwa na mwingine.
Kupitia SMS

Kama kweli unampenda, mpatie nafasi amalize masomo, kabla ya kuchafua akili yake na masuala ya mahaba.
Naogopa lakini namtaka

 

Naogopa wa kando sababu nimeokoka
Nimeolewa na nina mtoto mmoja wa kike. Mume wangu ananipenda sana. Lakini kuna jamaa ana mke na mtoto mmoja alinipenda. Lakini hatujakutana kimwili. Tatizo ni kwamba naogopa sababu nimeokoka lakini nisipoona sura yake sina raha.
Kupitia SMS

Majaribu na vishawishi ni kawaida katika ndoa na hata mahusiano. Tofauti inakuja jinsi unavyosuluhisha roho yako na uweze kuishi na amani. Kitu gani hasa unachokosa kwa mumeo ambacho unadhani utakipata ukienda nje. Labda hilo ndilo swali kubwa la kujiuliza na ujijibu na kisha uamue.

 

Ana wivu ajabu
Nimeolewa na mume wangu ana mwanamke pembeni. Na akiniona na mwanaume anakasirika. Niko Mombasa.
Kupitia SMS

Ina maana mmeoana na nyote wawili mnachakachua nje? Hii ni ndoa ama maradhi?

 

Ni ugonjwa ama nini?
Mimi nina mke na umri wangu ni miaka 22. Nikirushana roho ni raundi moja tu. Huu ni ugonjwa ama uzima? Kupitia SMS

Kwa kweli hapo mwanangu siwezi kujua. Wewe wajielewa na mwili wako vyema zaidi.

 

You can share this post!

Rais wa zamani aanza kutumikia kifungo cha miaka 12 katika...

FBI wavamia ofisi ya wakili wa Trump kuhusu ulaghai na...

adminleo