• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:50 AM
Kocha mpya wa Simbas atambulishwa

Kocha mpya wa Simbas atambulishwa

Na GEOFFREY ANENE

KOCHA mpya wa timu yake ya raga ya wachezaji 15 kila upande almaarufu Simbas, Ian Snook, ametambulishwa rasmi kwa umma jijini Nairobi, Alhamisi.

Raia wa New Zealand, Snook ameajiriwa kwa kandarasi ya mwaka mmoja. Atafanya kazi na raia mwenzake wa New Zealand, Murray Roulston pamoja na Wakenya Wangila Simiyu, Charles Ngovi, Christopher Makachia, Richard Ochieng’ na Dominique Habimana.

Snook na Roulston waliwasili nchini Kenya hapo Aprili 9. Snook anajaza nafasi ya raia wa Afrika Kusini, Jerome Paarwater, ambaye Shirikisho la Raga la Kenya (KRU) lilimtema Desemba mwaka 2017.

Taarifa kutoka KRU zinasema kwamba majukumu makubwa ya raia hao wa New Zealand ni kuongoza Kenya katika kampeni ya kufuzu kushiriki Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza mwaka 2019.

“Wana ujuzi wa zaidi ya miaka 50 kati yao katika kazi ya ukufunzi katika viwango mbalimbali kutoka mataifa yanayokuwa na pamoja na timu ya taifa ya New Zealand,” KRU imesema.

Snook na Roulston watashughulikia idara za mashambulizi na ulinzi, mtawalia. Hata hivyo, Snook ndiye kocha mkuu.

Ratiba ya Simbas ya Kombe la Afrika (2018):

Juni 23 – Morocco vs. Kenya (ugenini)

Juni 30 – Kenya vs. Zimbabwe (nyumbani)

Julai 7 – Kenya vs. Uganda (nyumbani)

Agosti 11 – Kenya vs. Tunisia (nyumbani)

Agosti 18 – Namibia vs. Kenya (ugenini)

You can share this post!

Shujaa kumenyana na Tonga Kombe la Dunia

GOLD COAST AUSTRALIA: Matokeo ya aibu kwa Kenya mita 400...

adminleo