• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
COTU na FKE zatisha kujiondoa NSSF

COTU na FKE zatisha kujiondoa NSSF

Na BERNARDINE MUTANU

MUUNGANO wa Vyama vya Wafanyikazi (COTU-K) na lile la waajiri (FKE) limetishia kujiondoa katika Hazina ya Kitaifa ya Malipo ya Uzeeni (NSSF).

Hii ni baada ya kugundua kuwa baadhi ya maafisa wa NSSF walikuwa wakilenga kubadilisha Sheria ya NSSF 2013, hata kabla ya utekelezaji wake kuanza.

Kulingana na taarifa iliyoandikwa na Katibu Mkuu wa COTU Francis Atwoli, mashirika hayo mawili, ambayo ni washirika wakuu wa NSSF hayajahusishwa katika mpango huo.

“COTU-K inapinga mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya NSSF 2013. Ni kinyume cha Katiba kufanyia marekebisho sheria ya NSSF bila kuhusisha COTU na Shirikisho la Waajiri (FKE),” ikasema taarifa hiyo.

Kulingana na Bw Atwoli, pesa zilizoko NSSF zimetoka kwa wafanyikazi na waajiri wao, na haiwezi kuwa wahusika wanaweza kuunda sheria bila kushirikisha COTU na FKE.

“Mpango huo ni kumaanisha kuwa wafanyikazi na waajiri hawana maana. Ikiwa wanachanga au la haijalishi kwa sababu kuna mtu anayefanya uamuzi kuhusiana na matumizi ya hazina hiyo bila idhini ya wafanyikazi na waajiri,” alisema Bw Atwoli.

Kulingana naye, haelewi ni vipi marekebishoo hayo kufanywa licha ya kuwa sheria hiyo haijaanza kutekelezwa.

“Bado sheria hiyo imo mahakamani kwa sababu ya maazimio ya watu wachache wanaotaka kuirekebisha tena,” alisema katika taarifa iliyotumwa katika vyombo vya habari.

COTU inataka kushauriwa kabla ya marekebisho yoyote kufanyiwa sheria hiyo la sivyo pamoja na FKE iunde mradi wa pensheni wa pamoja ambao utasimamiwa na vyama hivyo.

You can share this post!

Familia ya Moi iheshimiwe, viongozi waionya Jubilee

Kujiuzulu kwa Chebukati kutampa mwanya Chiloba kurejea IEBC...

adminleo