• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 8:50 AM
Boris Johnson agundulika ana virusi vya corona

Boris Johnson agundulika ana virusi vya corona

Na MASHIRIKA

LONDON, UINGEREZA

WAZIRI Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amesema vipimo vimebainisha ana virusi vya corona; ameweka maelezo katika ukurasa wa akaunti yake ya Twitter.

“Kwa kipindi cha saa 24 nimekuwa na dadili dhaifu za virusi vya corona na vipimo vimebainisha ni kweli ninavyo,” ameandika Johnson.

Kiongozi huyo amesema anajitenga, lakini akaondoa hofu akisema kwamba ataendelea kuiongoza serikali na kusimamia mchakato wa kukabiliana na maradhi ya Covid-19 kupitia makongamano ya video.

  • Tags

You can share this post!

CORONA: Mwanamke aliyetengwa kwa lazima ‘ajitia...

Mbunge atoa Sh5 milioni na mitungi 200 ya maji kukabiliana...

adminleo