• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:50 AM
Waliojaribu kuuzia polisi pembe huru kwa bondi ya Sh1m

Waliojaribu kuuzia polisi pembe huru kwa bondi ya Sh1m

Na HILLARY OMITI

MAHAKAMA ya Migori Jumatatu iliwaachilia watu wawili kwa dhamana ya Sh1 milioni kila mmoja, baada ya kukanusha kupatikana wakiwa na pembe za ndovu yenye thamani ya Sh1.5 milioni.

Hakimu Mkazi wa Migori, Bw Edwin Nyagah aliambiwa kuwa Mary Owino Likowa na George Ochieng walikamatwa Jumapili wakiwa na pembe hizo za uzani wa kilo 15.

Mahakama iliambiwa washtakiwa walikuwa katika kituo cha mafuta mjini Migori walipojaribu kuziuzia polisi wawili waliokuwa wamevaa kiraia na kujifanya wanunuzi baada ya kupata ujumbe kutoka kwa umma.

Kesi yao itasikizwa Juni 6 mwaka huu.

 

You can share this post!

Karua ataka korti iagize upya vifaa vya kura Kirinyaga...

Agizo picha za walaghai wa umeme zisichapishwe

adminleo