• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Wanachuo kizimbani kwa kuwapora wawekezaji wa Uchina mamilioni

Wanachuo kizimbani kwa kuwapora wawekezaji wa Uchina mamilioni

Na RICHARD MUNGUTI

WANAFUNZI wawili wa chuo kikuu kimoja jijini walioshtakiwa Jumatatu walidaiwa ni wanachama wa genge la majambazi linaloongozwa na mwanamke Mkenya Levanda Akinyi Ogilo na wanawake wengine wawili raia wa Tanzania.

Kiongozi wa mashtaka Solomon Naulikha alimweleza hakimu mkuu Francis Andayi kwamba kesi tano walizoshtakiwa Tolbert Ouma Odhiambo na Don Odhiambo Ogutu (pichani) zitaunganoshwa na zile walizoshtakiwa Akinyi na wenzake.

Sasa kesi dhidi ya Odhiambo na  Ogutu zitaunganishwa na zile dhidi ya Akinyi alyeishtakiwa pamoja na raia watatu wa Tanzania Bi Teresa Richard , Bi Rose Richard, na Shimton Ambasa Khan.

Washtakiwa wanadaiwa waliwalenga wawekezaji kutoka Uchina pesa na mali ambayo thamani yake ni zaidi ya Sh8.4 milioni .

Bi Levanda Akinyi Ogilo alifikishwa kortini baada ya hakimu mkuu wa Nairobi Bw Andayi kuwaamuru polisi wamfungulie mashtaka baada ya kumzuia rumande kwa muda wa wiki moja.

Bi Akinyi alishtakiwa pamoja na raia watatu wa Tanzania Bi Teresa Richard , Bi Rose Richard, na Shimton Ambasa Khan.

Washtakiwa hao walikabiliwa na mashtaka zaidi ya kumi ya kuvunja nyumba na kuiba mali na pesa kutoka kwa Mabw Zhang Gong , Wan Baihui, Bi Zhia Qian, Moses Kironyo Pratt na  Mohamud Hussein Egeh.

Washtakiwa hao wanne walikana kuiba Vipakatalishi, Dola za Kimerekani, Euro na sarafu za Uchina zote zenywe thamani ya zaidi ya Sh8,463,000.

Wakili John Swaka anayewakilishtakiwa hao wote aliomba mahakama iwaachilie kwa dhamana akisema Akinyi ni mama aliyeacha watoto kwa nyumba.

Bw Swaka alisema washtakiwa hao walitiwa nguvuni Machi 30, 2018 na wamekuwa wakizuiliwa katika vituo mbali mbali vya polisi.

Hakimu Mkuu akisikiza kesi hiyo. Picha/ Richard Munguti

Jambo hilo lilimuudhi Bw Andayi ndipo akamwagiza kiongozi wa mashtaka Bw Solomon Naulikha apeleke uamuzi wa mahakama kuu katika kila kituo cha polisi jijini Nairobi unaosema hakuna mshukiwa wa wizi au kosa lingine lolote anayepasa kuzuiliwa kama hakuna shtaka la kushikilia.

“Lazima maafisa wote wa polisi wafahamishwe kwamba lazima wawasilishe kortini shtaka la kushikilia ndipo wakubaliwe kumweka rumande mshukiwa wakimhoji,” aliamuru hakimu.

Bw Andayi aligadhabishwa na tabia ya polisi ya kuwazuilia washtakiwa kwa siku nyingi kabla ya kuwashtaki.

Washtakiwa hao walikuwa wakizuiliwa katika kituo cha Kilimani kwa zaidi ya siku saba polisi wakiandikisha taarifa za mashahidi.

Akiomba washtakiwa hao wazuiliwe kuhojiwa na kuwasaidia polisi kutambua wanakoweka bidhaa walizoiba , hakimu alifahamishwa washtakiwa hawa hutorokea Tanzania.

“Punde tu washukiwa hawa wanapotekeleza uhalifu wanatorokea nchi jirani ya Tanzania,” alisema Konstebo James Wanjohi wa idara ya upelelezi.

 

CCTV

Hakimu alifahamishwa kwamba washukiwa hao wametambuliwa katika picha za CCTV ambapo wanaonekana wakiwa wamejihami na bastola.

“Punde tu wanapotekeleza uhalifu washukiwa hawa hutorokea nchi jirani ya Tanzania,” alisema Bw Wanjohi aliyeongeza , “ kwa muda wa miaka mitatu tumekuwa tukichunguza mienendo ya washukiwa hawa watano.

Mahakama ilifahamishwa washtakiwa walitekeleza wizi huo katika mtaa wa Kilimani Nairobi miezi ya Feburuari na Machi 2018.

Waliachiliwa kwa dhamana ya kati ya Sh300,000 hadi  Sh1milioni pesa tasilimu hadi. Akinyi atalipa zaidi ya Sh3milioni ikiwa atafaulu kulipa dhamana hiyo ndipo aachiliwe. Anakabiliwa na kesi tano tofauti.

Kesi zitasikizwa kati ya Mei 3 hadi 10 mwaka huu.

You can share this post!

Motoni kwa ulanguzi wa wasichana kutoka Burundi

BI TAIFA MACHI 09, 2018

adminleo