• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 10:15 AM
Polisi aliyemuua mwanafunzi azuiliwa

Polisi aliyemuua mwanafunzi azuiliwa

Na Richard Munguti

Mahakama Kuu Nairobi Alhamisi iliamuru afisa wa polisi Emmanuel Abunya azuiiliwe hadi Aprili 23 2020 atakaposhtakiwa kwa mauaji ya Carilton Maina miaka miwili iliyopita.

Maina alikuwa mwanafunzi wa chuo kikuu cha Leeds nchini Uingereza.

Jaji Ngenye Macharia aliagiza Abunya apelekwe kupimwa akili katika hospitali ya Mathari.

Upande wa mashtaka uliomba afisa huyo asikubaliwe kujibu shtaka kwa vile utimamu wa akili yake haujulikani.

Wakili Harun Ndubi anayemwakilisha Abunya aliomba mshukiwa aachiliwe kwa dhamana lakini upande wa mashtaka ukapinga.

Jaji Macharia alimweleza mshukiwa atajibu shtaka la kumuua Maina Desemba 22, 2018 mnamo Aprili 23.

You can share this post!

Waliopatikana na simu ya polisi aliyetoweka watupwa ndani

Mkenya anayeishi Dubai asema bila kuvalia barakoa na glavu...

adminleo